TUMEUMBWA
KUISHI ndani ya NAFASI ZETU, kilammoja.
Usahihi wa kila kitu tunachofanya umebebwa na NAFASI tunayoitumia kufanyia chochote
kile.
Ninaamini kuwa moja kati ya sababu kwanini maombi yetu
hayajibiwi kwa wakati au hayajibiwi kabisa ni kuomba tukiwa NJE YA NAFASI ZETU.
NAFASI
NI NINI?
Nafasi ni eneo ambalo mtu amepewa, au fursa au cheo ambapo
mtu aliyepewa anatakiwa kufanya mambo yakeyote au KUISHI MAISHA YAKE YOTE akiwa hapo. KILA ANACHOFANYA LAZIMA KIFANYIKE TOKEA KWENYE NAFASI YAKE.
NAFASI
imebeba KILA KITU.
NAFASI
imebeba HATMA.
NAFASI
imebeba KIBALI.
NAFASI
imebeba KANUNI.
NAFASI
imebeba FURSA.
NAFASI
imebeba WATUNA
RASLIMALI zote unazohitaji kufanikiwa.
NAFASI
imebeba UPENYO.
NAFASI
imebeba MAFANIKIO YA
KWELI.
NAFASI
imebeba MAJIBU SAHIHI.
NAFASI
imebeba SILAHA.
Mwanzo 3:9
Bwana
Mungu akamwita Adamu, akamwambia, ukowapi?
Tunaona katika Mwanzo 3:9, Mungu anamuuliza Adamu, UKO WAPI-WHERE ARE YOU?
Hili ni swali la NAFASI-POSITION.Tungetegemea
Adamu angeulizwa UMEFANYA NINI.....lakini
hakuulizwa hivyo, kwasababu, UNACHOFANYA
KIMEFUNGWA KWENYE NAFASI......
Kwa lugha ingine, Mungu anajaribu kuonesha hapo kuwa Adamu
angekuwa kwenye NAFASI YAKE asingekosea
kwakumkubali mkewe kula tunda alilokatazwa. Kumbuka ADAMU HAKUDANGANYWA NA NYOKA BALI EVA. Aliye danganywa ni Eva,
ndiye alianza kukosea lakini Mungu alipokuja hakuuliza EVA UKO WAPI kwani kila mtu ana nafasi yake. ADAMU NI KIONGOZI KATIKA UONGOZI, EVA NI KIONGOZI KATIKA USAIDIZI.
ADAM
IS A LEADER IN A LEADING ROLE AND EVE IS A LEADER IN A HELPING ROLE. THEY ARE
ALL LEADERS BUT IN DIFFERENT POSITIONS.
Eva asingekosea kama ANGESIMAMA
na KURIDHIKA na NAFASI YAKE yakuwa
MSAIDIZI WA KUMFAA ADAM. Ila tunaona
wote wawili walikosea. Eva alikosea kwakuwa alitoka NJE YA NAFASI YAKE. Na Adamu alikosea pia kwa kutoka nje ya NAFASI YAKE....How?
Eva alipofuatwa na nyoka alitoka kwenye nafasi yake kwa UJUAJI WAKE.
Adamu alitoka kwenye nafasi yake na akala tunda kwa HURUMA ZA KIMAPENZI KWA MKEWE.
Eva angebaki kwenye NAFASI
yake kama angemwambia nyoka, SIWEZI
KUKUJIBU MPAKA KIONGOZI WANGU AWEPO.
Adam asingekosea kama ANGEMSIMAMIA
VIZURI mkewe.
KILA
MTU ALIKOSEA AKIWA NJE YA NAFASI,
lakini Mungu alipokuja akamuuliza KIONGOZI-MUME....UKO
WAPI....Mungu hakuuliza“MKO WAPI?”
DIVORCE
nyingi zinatokea kwasababu kila mtu anakuwa NJE YA NAFASI yake.....
Wanawake wanataka kuishi na kuwa kama wanaume. Wanaume wanataka
kuishi nakuwa kama wanawake.
MAHUSIANO
MENGI YAMEKAA KISHINDANI.
NDOA
NYINGI ZIMEKAA KISHINDANI KWANI KILA MTU ANATAKA KUFANYA AFANYALO NJE YA NAFASI
ALIYOPEWA.
Kukaa na kuishi nje ya NAFASI
ndio msingi wa uharibifu wa mambo mengi sana mpaka leo.
UKO
WAPI? Hili ni swali gumu sana. Na
ukisoma Biblia utaona watu hutoka kwenye nafasi zao kidogokidogo. Lakini sababu
kubwa ni pale mtu anapo fika na KUMKATAA
MUNGU KATIKAFAHAMU ZAKE. Yaani kutokukubali MAMLAKA ya Mungu ifanye kazi ndani yake. Kutaka uhuru usio na mipaka.
Warumi
1:24-27
“Kwa ajili
yahayo Mungu aliwaacha katika tamaa za mioyo yao, waufuate uchafu, hata wakavunjiana
heshi mamiiliyao. Kwa maana waliibadili kweli ya Mungu kuwa uongo,
wakakisujudia kiumbe na kukiabudu badala ya Muumba anaye himidiwa milele. Amina.
Hivyo Mungu
aliwaachia wafuate tama zao za aibu, hata wanawake wakabadili matumizi ya asili
kwa matumizi yasiyo yaasili; wanaume nao vivyohivyo waliyaacha matumizi ya mke,
ya asili, wakawakiana tama, wanaume wakiyatenda yasiyo pasa, wakapata nafsini mwao
malipo ya upotevu wao yaliyo haki yao.”
Unaona hapo WALIVUNJIANA
HESHIMA MIILI YAO.....maana yake walianza kuitumia miili yao kinyume na namna
ilivyo umbwa na vile inavyo takiwa kutumika. KINYUME NA MAUMBILE. USHOGA NA USAGAJI.
Ukiwa kwenye mahusiano na kila kitu unataka kifanyike unavyotaka
wewe ujue wewe ni MSHINDANI na sio MKAMILISHAJI.....YOU ARE THERE TO COMPETE,
NOT TO COMPLETE.
NAFASI
IMEBEBA USHAWISHI.
Kukaa nje ya nafasi zetu, ndio kinatufanya hata tunapo omba tuna
omba kama Mungu ni msela wetu mpaka wakati mwingine TUNAMFOKEA kabisa.
Mtoto anae jua nafasi yake kwa Baba yake, anapokuwa anaomba kitu
huwa anakuwaje vile?
Kuto kujua nafasi zetu kumetufanya sisi tulio watoto wa mfalme
tuishi kama watumwa na watumwa wandundatu kama watoto wa mfalme. ASANTE UJINGA.
Huwa tunatolewa nje ya nafasi zetu kwa NGUVU YA USHAWISHI inayo changanyika na kiwango Fulani hivi cha
ujinga.
Quote by Raphael JL
“Ushawishi
wowote kazi yakeni KUUGEUZA MOYO kuelekea
kule ambako mshawishi anataka, yaani kubadili mfumo mzima wa kufikiri na kuamua
kwa mtu ili aweze kufanya kinyume na alivyo kuwa mwanzoni. Kila ushawishi una NIA-ROHO nyuma yake. INFLUENCE IS A FUNCTION OF MOTIVE.”
Ndio maana utaona watu wengi, hata mahusiano mengi huwa yanaharibika
Zaidi kwa ushauri wa nje kutegemea ushauri huo unatoka wapi.
Mithali
1:10
“Mwanangu,
wenye dhambi wakikushawishi, wewe usikubali”
Kwenye eneo la ndoa, kwa mfano.....kinafasi, A MAN IS A LEADER. A WOMAN IS A HELPER.....kila
mtu mwenye kutaka kufurahia ndoa yake lazima aanzie hapo, ni hatari kugombania nafasi
ya mtu mwingine.
NAFASI
IMEBEBA WAJIBU.
Wewe jiulize kama Adamu angewajibika. Kama Eva angewajibika.
Au kama wewe ungewajibika kwenye nafasi yako, mngepigana vibuti? Mngeachana?
NAFASI
IMEBEBA UFAHAMU.
Mwanzo
3:9
Bwana
Mungu akamwita Adamu, akamwambia, ukowapi?
Kuna mahali au kuna nafasi Mungu alimpa Adamu.....UKO WAPI.....ni kama Mungu anasema.....Adamu
kuna nafasi nilikuweka mbona sikuoni?
Kuna watu wanakuja kwenye maisha yetu ili TUWASAIDIE waweze kupiga hatua,ila kwakuwa
huwa hatujui nafasi zetu unakuta watu wanaishia kutongazana, kwanini usipigwe kibuti?
Mtu amekuja ili awe mwanafunzi na mfuasi wako katika Bwana, wewe unaanza kuleta
stori za mapenzi.laiti kama tunge jua ndo maana kuna watu unaweza hata usijue lini
walipoteana kuondoka karibu yako....kumbe ulianza kuongea pumba nje ya nafsi yako.
kuna nafasi aliyonipa mungu kwenye
mahusiano yangu na wewe. kuna nafasi
natakiwa kumpa mungu ndani yangu. kuna
nafasi yangu kwa mke wangu. kuna
nafasi yangu kwa watoto wangu. kuna
nafasi yangu kazini. kuna nafasi
yangu kanisani.
Muheshimu mtu ambaye unajua amekupa nafasi ambayo neon lako moja
linaweza kuathiri maisha yake yote. JE MUNGU SI ZAIDI?.
STAND IN YOUR POSITION!
SIMAMA KATIKA NAFASI YAKO!
0 comments:
Post a Comment