DESTINY (HATMA) ni mwisho wa jambo,kwa tafisiri nyepesi na ya
kawaida sana, bila kuyakuza mambo. Hatma ni mwisho wa mwelekeo wang au wako.
Kila jambo lenye mwanzo lina hatma katika tamati yake. Hata kwenye mahusiano
pia. Nini hatma ya mahusiano yako? Unaweza usijue nini hatma ila lazima ipo na
hiyo hatma inaathiriwa na mambo kadhaa ambayo kwa sehemu ndio tunajifunza leo
kwa kutumia kanuni tatu au zaidi kwa pamoja.
Zipo kanuni zinaweza kukusaidia kuwa
mahusiano mazuri na ya kufurahisha kama ukiamua.
Kanuni ya
Kwanza_: KANUNI YA USAHIHI.
Hii ni kanuni kubwa
sana kwenye mahusiano.usahihi ni maamuzi, yaani ukishajua uliye naye ni mtu
sahihi unakuwa na ushindi wa asilimia 20 hivi.
KWENYE USAHIHI
UNAJIULIZA MASWALI KADHAA
1. WEWE NI SAHIHI
KWAKE?
2. YEYE NI SAHIHI
KWAKO?
Kikubwa cha kuelewa hapo ni kuwa usahihi
umefungwa kwenye nani na sio nini.its all about WHO and not WHAT.lazima wote
muwe sahihi japo asilimia 20 za usahihi haziondoi asilimia 80 za kuwajibika.
Ni rahisi sanaa
kuishi na mtu asiye sahihi nakwambia.asilimia kubwa sana ya watu wasio sahihi
huwa ni wakamilifu sanaa na pretenders wa kutupwa.
Watu wasio
sahihi hujitahidi sana kukaa mahali sahihi lakini kwa kuwa wao sio sahihi
jitihada zao huwa hazidumu kwa mtu mwenye uelewa.
· Shauku yako ya
kupatia haitakiwi kuzidi kusudi lako la kufanya, kuwa au kujua vinginevyo
utajikuta umekosea zaidi ya kiu yako ya kupatia
·
Usahihi hauondoi
changamoto au madhaifu
·
Kumpata mtu sahihi
kwenye maisha yako ambaye ndo unaamini unaenda kuanza nae maisha ya ndoa
hakuondoi changamoto za yatokanayo na nyie wawili.
·
Japo kwamba ni mtu
sahihi lakini bado usahihi ni wa ule uchaguzi ulioufanya wa kumchagua yeye na
sio wa kuondoa changamoto au udhaifu.
·
Wengi husahau kuwa
ni kweli ni sahihi lakini bado ni mwanadamu, bado ana mapungufu,bado ana
madhaifu ya kutosha tu, anaweza akawa sahihi na bado akawa mjinga, akawa
mshamba, akawa sio wa kiroho kwa vipimo vyako lakini ni sahihi.
·
Hakuna mtu huwa
anataka wala kutamani kukosea kwenye mipango na ndoto zake lakini,
·
Bahati mbaya sana
ile hali ya kutaka kupatia sana hata kuwa tayari kutokujali kuhusu kusudi la
jambo lenyewe husababisha ndani yetu mawazo, mchanganyiko kwa namna ambayo
wengi hujikuta hawajui nini la kufanya lakini huamua kufanya ambalo linaleta
ladha ya wakati kwa mihemko ya hofu au mashaka au wasiwasi.
·
Kupatia kuoa na
kupatia kuolewa ili mpatie kuoana, lakini nataka muone upande wa pili wa shauku
hii ambayo inaweza kukuharibu pia. Ni kama vile kusema,asali ni tamu lakini
ukiila kwa kuzidi inaweza kukuharibu. Kazi ya Mungu inaweza kuharibu mahusiano
yako na Mungu usipokuwa makini.
·
Usipojua hilo na
usipojua namna ya kuishi na mtu sahihi lakini mwenye mapungufu unaweza
ukajikuta hakuna mahusiano yanayokufaa maana cha ajabu kabisa utakuwa
hujui shida iko wapi huku ukijihesabia haki kuwa wewe uko sahihi.
·
Usahihi wake uko
kwenye hatma lakini sio kwenye maisha ya kila siku ambayo ndio unatakiwa
ujifunze ili ujue kuwa usahihi hauondoi nafasi ya kujifunza ili uwe bora zaidi
·
Mungu anaweza kabisa
kukuonyesha kuwa fulani yule ndo mumeo au mkeo lakini umbali wa kutoka kwenye
kuonyeshwa mpaka kwenye uhalisia wa maisha halisi unaweza kukuvugura mpaka
ukabaki huna hamu na mahusiano milele.
·
Hii ni kwasababu
kuonyeshwa ni jambo moja, lakini pia Mungu huonyesha utukufu wa mwisho ila
mchakato wa namna ya kuishi huwa unabaki mikononi mwako moyoni mwake Mungu.
Kuingia kwenye
mahusiano na mtu sahihi ni moja ya changamoto kubwa sana kwenye mahusiano ya
siku hizi maana ni kama vile usahihi wenyewe haujulikani.
JIULIZE MWENYEWE, NANI KAKUFUNDISHA USAHIHI?
NANI ALIKUFUNDISHA
USAHIHI? NANI ALIKUFUNDISHA KUHUSU MAHUSIANO? NANI ALIKUFUNDISHA NAMNA YA
KUPATA JIBU SAHIHI? UNA PICHA GANI YA NDOA YAKO? UNATAKA NINI NA UMEJUAJE
UNATAKA UNACHOTAKA? INFORMATION.....NAWASAMEHE MAKUNGWI KADHAA KWENYE HILI.
Kanuni ya pili: KANUNI YA KUISHI NDANI AU KATIKA USAHIHI
Asilimia kubwa ya
watu wanaishi katika hali ya kutokuwa sahihi na wanategemea watu
sahihi.unatakiwa uishi katika level ya usahihi in a way mtu sahihi akikuona
anaweza kukutambua.be honest to yourself.
Mfano: unategemea
kwenda Sumbawanga.kujua unatakiwa kwenda Sumbawanga it's who part, nani unaenda
nani? Njia unajua? Its how part.
Kuna vitu vingi
usipojua kabla hujaingia kwenye ndoa unaweza kuacha ndoa usiku wa honeymoon.
Ukimkubali mtu maana
yake ni mtu sahihi ina maana kwamba umekubaliana na madhaifu yake. Mfano
ukipeleka jambo la kuoa nyumbani lazima muwe mmetengeneza oneness.in a way
mnaweza kuwatengeneza wengine wakakubaliana na nyie. Ukishajitambua who
are you mambo mengine yote unaweza kudeal nayo.
Sio mahusiano yote
yanayovunjika hayakuwa sahihi mengine ni namna ya kushindwa kuishi katika
usahihi.
We are living in
information age.
Unaweza kukusanya
taarifa sahihi ila namna unavyozitumia zikaleta athari kubwa.
Mahusiano mengi
yanafunjika sababu ya tafsiri mbaya ya taarifa.
Nyie wawili ndio
chanzo cha taarifa so hakikisheni mnazichuja vizuri.
Serikali yenyewe ina
msemaji mkuu same applied kwenye mahusiano yenu.
Kiongozi ni kiongozi
na msaidizi ni msaidizi. Lazima ujue jinsi ya kupokea taarifa na
kuzimeng'enya.
Taarifa ni chanzo
kizuri mno cha kuharibu mahusiano.
KWENYE KIOO UKIWA
UMEFUMBA MACHO.
Ili uweze kujiangalia
ni lazima uweze kujitazama, fumbua macho.usijiangalie wakati macho yamefungwa.
Wazo la kanuni hii
ni kuwa usijidanganye, usijitie moyo.
Huna cha kupoteza,
huna cha kuficha kama umejikubali kwenye hayo mahusiano.
Tafuta
taarifa. Hakikisha unafungua macho.
Jikague mwenyewe
kwanza.be honest to yourself.
Kuwa accountable kwa
kila unachofanya.chukua wajibu na wajibika.
Kanuni ya tano: KANUNI YA KUUAMINI
UPEPO KATIKA SAFARI MOJA.
Sifa ya upepo
hautabiriki, haupangiki na wakati wowote unaweza kubadili mwelekeo.
Kwa kusema haya
namaanisha usimwamini mtu ambaye hana mwelekeo wa maisha, hana vision, hajui
matumizi mazuri ya kile ambacho anacho.
Kutembea na mtu wa
aina hii itakusababisha kutumia nguvu nyingi sanaa kuyalinda hayo mahusiano.
Ili kuwa na
mahusiano mazuri lazima muwe na maono yanayofanana.
Msipokuwa na
kuelewana ndo ile utaishi na mtu upepo. analala Leo hajui kesho atafanya
nini.anasikia jambo mahali linambadili mwelekeo.
Kuendelea kukaa
kwenye hayo mahusiano ni maamuzi pia.
Lazima mtembee
katika kusudi linalofanana. Shikaneni mikono mtembee pamoja.make sure
umemwamini mtu sahihi.
Kanuni ya sita: KANUNI YA KUJIOGOPA KWA KUMUOGOPA ANAEKUOGOPA
Kanuni ya saba: KANUNI YA KUKATAA UNAYOYATAKA KWA KUYAKUBALI.
Kwenye mahusiano
lazima ujue unachotaka ili ikusaidie kupata unachotarajia ili kikija ambacho
hukutarajia iwe ni kwasababu nyingine na sio wewe mwenyewe kutokujua
unachotaka.unachotaka unaweza kuwa unachostahili kama ukipatia katika kuwa
mkweli kwa unachotaka pia.
Kanuni ya nane: KANUNI CHA KUCHIMBA
KISIMA SIKU UNA KIU.
Wazo la kuchimba
kisima wakati una kiu.kiu ni uhitaji.ukichimba kisima wakati una kiu utachimba
kisima kwa pressure na hata energy yako itatukuwa kubwa.
Kuchimba kisima
wakati una kiu kunaweza kusababisha ukasahau mambo ya msingi.
Kuchimba kisima
wakati una kiu ni reactive response ambayo most on ladies wanakuwa nayo wen
comes to relation don’t rush into relation because there is price to
pay.when you say yes there will be price to pay and vice versa.
When a man comes u
must make sure your in the same response as his.dont rush.
Usitengenezewe wala
usijitenge uhitaji.ukitengenezewa na ukitengeneza zote ni external.its should
be internal.should comes from within you.
Knowing that when u
agree to be in relation u agree with anything concerning him including
his family, friends etc.
Wacha maturity and
growth take you to relation.
Wacha
kuparamia.utakuja paramia mtu kavaa koti la upupu.
Ukisoma mwanzo
utaona Mungu ndo aliona uhitaji wa Adam kutaka msaidizi na wala sio uhitaji wa
Adam.
Kuna aina fulani ya
baraka huwezi kuzipata hadi uwe umekuwa.
Kanuni
ya tisa
KANUNI YA KUMHURUMIA ANAEKUUMIZA KWAKUWA
ANACHEKA ILI USIVUNJE AGANO LAKO.
Moja kati ya
changamoto kwa Adam wa kike ni kujihurumia.kuogopa kumpoteza, kila kitu ni
kuogopa na kujihurumia mpaka unakuta unaishi kama mkimbizi kwenye mahusiano
ambayo ulikuwa unayaota kwa sababu unatarajia tu kuwa one day itakuwa sawa.
Ambacho unaweza ukawa huelewi wewe Adam wa kike ni kuwa hofu yako ya
kujihurumia inaweza kukusababisha ukazidi kukosea zaidi kila siku.unaogopa
kumuumiza anaekuumiza kwa gharama ya wewe kuendelea kuwa mtumwa wa maumivu
yake? Na ndio maana wengi wanasema Mungu ana majibu matatu.kazi kweli kweli.
UKIUMIA KWA
KUJITAKIA USILIE. VUMILIA TU haha ha ahahahahah.
Ni aibu kubwa sana
kumsinguzia shetani kosa ambalo ulishiriki kwa asilimia 75.unapata wapi ujasiri
wa kusema shetani alijiinua? Hujui ndio tabia yake kujiinua na ndo maana Bwana
alishamshusha?
NB Kuishi na kosa ni mateso makubwa kuliko
kuchelewa kuolewa.
Kuishi na kosa ni lile wazo la kuingia kwenye
ndoa kwa sababu za kipuuzi.
Kupotea kuna raha
yake haswa ukipotea mchana.raha ya kupotea ni kuendelea kupotea ukiamini bado
kidogo utapata njia sahihi na kumbe suluhisho pekee ni kurudi ulipotoka na
kuanza upya.
Safi Mtumushi ujumbe mzuri
ReplyDeleteAminaa
Delete