Mungu kwanza

Tuesday 18 June 2013

UMUHIMU NA NAMNA YA KUISHI MAISHA YA MAOMBI

Kuna umuhimu mkubwa sana kama mkristo kuishi maisha ya maombi,maombi ndiyo siraha pekee kwa mkristo,kuishi maisha ya maombi kunakuimarisha Kiroho na kujenga matumaini yako kwa Mungu wako.Kumbuka kama mkristo kuishi bila kuwa na maombi kwenye maisha yako nisawa gari lisilo kuwa na Injini.
        Inawezekana unajua maana nyingi za maombi lakini hujui namna na umuhimu wa kuishi maisha ya maombi,kujua maana ya maombi siyo tatizo ila tatizo ni kwamba watu wengi hawajui kuishi maisha ya maombi.Maombi ni njia aliyo jichagulia Mungu kufanya kazi duniani kupitia wanadamu.hakuna kitu chochote kinacho weza kufanyika duniani pasipo maombi,maombi ndiyo kiunganishi pekee kati ya Mungu na wanadamu.kama ni msomaji mzuri wa Biblia utajua kuwa hatuna karama ya maombi kama zilivyo karama nyingine katika Biblia.Maombi ni ya kila mtu.Huduma ya maombi ni ya kila mtu,na tena maombi hayo yanzie ndani ya moyo wako.Maombi ni agizo lilo tolewa na Mungu kuhusu kitu fulani na huwa unaagizwa kuomba.


 Nini maana ya Maombi?.
     Maombi ni mfumo alio utengeneza Mungu mwenyewe kufanya kazi pamoja na wanadamu duniani,kwahiyo kama maombi ni mfumo basi usiya fanye maombi kuwa sheria,ukiyafanya maombi yawe sheria huwezi kuishi maisha ya maombi katika maisha yako,ukinjiwekea sheria kwenye maombi huwezi kuomba ukiwa eneo njingine.Mfano watu wengine huwa wamejiwekea sheria kuomba wakiwa maeneo fulani.Roho mtakatifu ni muhimu sana kwenye maisha ya maombi maana yeye ndiye anaye tuombea kwa kuugua,Roho mtakatifu ni kiongozi wako na anafuata unacho mwagiza na anafanya,kwa namna hii huwezi kuomba pasipo Roho mtatifu ndani yako.Hapo awali nimekuambia maombi ni mfumo na siyo sheria au kanuni,Naombi siyo mfumo wa mtu bali ni mfumo wa Mungu mwenyewe

.
Note;Ukiona maombi yanakuwa mzigo kwako ujue Roho mtakatifu hayupo hapo,maombi yafanye ni starehe utajisikia roho yako kuwa kwenye laini ya maombi kila wakati.Kumbuka hakuna huduma ya kimungu inayo weza kufanyika pasipo maombi,Huduma zote unazo zifahamu zinategemea sana maombi na mwombaji ni wewe.
Share:

Contact

P.o.Box 1404 Mwanza Tanzania
E-mail : frhebron@yahoo.com , frhebron@hotmail.com
Mobile: +255716 423 428 , +255766 710 028

Website Visitors

Copyright © Hebron Fredrick All Rights Reserved Designed and Developed by Hebron Fredrick+255716 423 428