Mungu kwanza

Sunday 16 January 2022

TUMETOKA MBALI........!!



Kuna watu wana marafiki na wanasema wametoka mbali sana lakini cha ajabu hawajawapeleka mbali.....

Tangu rafiki yako awe fulani hata ibada umeacha,huwezi kuomba tena,umekuwa na tabia mbovu...

Tangu rafiki yako awe fulani huna heshima kwa mkeo na wala hujali kuhusu familia yako na huyo rafiki ameshauri uwe hata na kamchepuko...

Tangu rafiki yako awe fulani mmeo unaongea naye vyovyote vile bila adabu na wala hujali,
Tumekazana kusema this is my best friend since primary since childhood lakini hajakufanya uwe bora....

Rafiki yako ana mitazamo mibaya kuhusu ndoa, wanaume, wanawake hana interest na mafanikio unadhani utakuwa salama?
Rafiki yako anakuambia unaishije bila demu,unaishije kuwa tu mke lazima uwe na mchepuko je unadhani utakuwa salama??

Ni rafiki yako lakini huwezi kumwambia ukweli akikosea au akifanya kitu si sahihi eti kwamba unatunza urafiki unaogopa atakuchukia that's not friendship...

Enenda pamoja na wenye hekima, nawe utakuwa na hekima; Bali rafiki wa wapumbavu ataumia.
Mithali 13:20
Ukiwa na rafiki mpumbavu jiandae kuangamia,
Unaweza kuangamiza ndoa yako, biashara, huduma kisa marafiki ulionao.

Nani ni rafiki yako?
Tangu uwe naye mmesaidiana kuwa bora?
Umemzidi kumpenda na kumheshimu Mungu?? Jiulize kwa upole.

Choose wisely. 
Share:

0 comments:

Post a Comment

Contact

P.o.Box 1404 Mwanza Tanzania
E-mail : frhebron@yahoo.com , frhebron@hotmail.com
Mobile: +255716 423 428 , +255766 710 028

Website Visitors

Copyright © Hebron Fredrick All Rights Reserved Designed and Developed by Hebron Fredrick+255716 423 428